Flag of Tanzania

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Language: English | Swahili

Speeches Shim

13-11-2020 01:15

DAR ES SALAAM, TANZANIA, Novemba 12, 2020- Mradi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) wa Kuendeleza Mazingira, Uhifadhi, na Utalii wa Tanzania (PROTECT) ulifanya kikao mtandao kilichorushwa mubashara kusherehekea miaka mitano ya kulinda baioanuai na uchumi unaotokana na utalii.

Hafla hiyo ya kidijitali, "Kuadhimisha USAID PROTECT: Miaka Mitano ya Kuhifadhi Wanyamapori wa Tanzania," ilionesha mafanikio ya mradi huo, pamoja na jinsi ulivyochangia kupunguza ujangili nchini kwa asilimia 80, kulingana na taarifa za Wizara ya Maliasili na Utalii.

"Kazi nyingi zilizofanywa na USAID PROTECT zitaacha msingi wa kudumu wa uhifadhi nchini Tanzania. Mradi huo umeshirikisha mashirika ya kitaifa na kampuni binafsi zilizopo nchini ili kupata ushawishi na mali zao katika juhudi za uhifadhi. Hii imesababisha kuhifadhiwa kwa zaidi ya hekta 300,000 za maeneo muhimu kibaiolojia na kupunguzwa kwa kiasi kikubwa cha ujangili na uvuvi usiodhibitiwa.”, alisema Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa USAID, V. Kate Somvongsiri, ambaye alifungua kikao mtandao hicho.

Serikali ya Marekani yaimarisha mifumo ya afya inayolenga kumaliza janga la VVU nchini Tanzania
17-07-2020 04:30

Dar es salaam: Julai 16, wawakilishi kutoka Serikali ya Marekani na Serikali ya Tanzania walishiriki katika kikao-mtandao ambapo walijadili mafanikio na hatua za kuchukua siku zijazo ili kuimarisha  mifumo ya afya nchini Tanzania, kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) na mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Afya na Ustawi wa Jamii (CHSSP).

Fedha hizi ni nyongeza ya msaada wa Dola za Kimarekani milioni 1 unaolenga kusaidia mapambano dhidi ya janga la COVID-19 uliotolewa hivi karibuni na kufanya kiasi kipya cha fedha zilizotolewa kwa Tanzania ili kukabiliana na janga hili kufikia Dola za Kimarekani milioni 3.4.
22-05-2020 08:30

Dar es Salaam: Marekani imetangaza kuwa kupitia Shirika lake la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) itaongeza kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 2.4 (Takriban Shilingi za Kitanzania bilioni 5.6), ikiwa ni msaada kwa sekta ya afya nchini Tanzania.  Msaada huu unalenga kuimarisha uwezo wa maabara na upimaji wa kimaabara (laboratory capacity for optimal diagnostics), kusaidia jitihada za utoaji taarifa (risk communication) , miradi ya maji na usafi wa mazingira (water and sanitation), kuzuia na kudhibiti maambukizi,  kutoa elimu ya afya kwa umma (public health messaging) na miradi mingine. Fedha hizi ni nyongeza ya msaada wa Dola za Kimarekani milioni 1 unaolenga kusaidia mapambano dhidi ya janga la COVID-19 uliotolewa hivi karibuni na kufanya kiasi kipya cha fedha zilizotolewa kwa Tanzania ili kukabiliana na janga hili kufikia Dola za Kimarekani milioni 3.4. Isitoshe, kiasi kingine cha Dola za Kimarekani milioni 1.9 zimebadilishwa matumizi na kuelekezwa kwenye mapambano dhidi ya janga hili. Hii inafanya jumla ya fedha zote zilizotolewa na Marekani katika kukabiliana na COVID-19 nchini Tanzania hadi hivi sasa kufikia Dola za Kimarekani milioni 5.3 (Sawa na Shilingi za Kitanzania bilioni 12.2).